FM Manyara

 NHIF yaboreha kitita cha mafao

April 9, 2024, 2:47 pm

Picha ya Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoa wa Manyara Joyce Sumbwe akiongea katika studio za Fm Manyara

Jamii mkoani Manyara imetakiwa kujiunga na mfuko Taifa wa bima ya Afya.

Na George Agustino

Jamii mkoani Manyara imetakiwa kujiunga na mfuko wa Taifa wa bima ya afya NHIF ili kuepuka gharama kubwa za matibabu wanapokwenda kupata huduma za matibabu katika hospital.

Meneja wa mfuko wataifa wa bima ya afya mkoa wa Manyara Joyce Sumbwe ameyasema hayo wakati akizungumza na Fm Manyara katika kipindii cha Mseto wa leo kuhusu kitita chaboreshwa mafao kilicho ndani ya mfuko huo, amesema ni utaratibu wa mfuko huo kuboresha huduma zao  ili kuendana na Teknolojia nakusaidia  kuondoa changamoto mbalimbali   wakati wa utoaji wa huduma za Afya kwa mnufaika.

Sauti ya Meneja wa mfuko wataifa wa bima ya afya mkoa Manyara

Aidha amesema hakuna gharama za ziada ambazo  mnufaika wa mfuko wa bima  ya Afya anatakiwa kulipa na ikitokea amedaiwa fedha anapokwenda kupata matibabu  anatakiwa kutoa taarifa kwa kupiga  simu namba ya huduma kwa wateja ambayo ni 199 ili kupatiwa msaada au kufika katika ofisi zao zilipo nchini nzima.