FM Manyara

Wagonjwa 10 wa kipindupindu waruhusiwa Mrara

March 8, 2024, 11:03 am

Picha Afisa Afya Emanuel Kimeonge na Mratibu wa elmu laurensia Urio Halmashauri ya mji wa Babati wakitoa elimu ya ugonjwa wa kipindu pindu katika kituo cha Fm Manyara.

Wagonjwa waliokuwa wanaugua ugonjwa wa kipindu pindu waruhusiwa baada ya kupatiwa matibabu.

Na Mzidalifa zaid

Wagonjwa 10 waliokuwa wanaugua ugonjwa wa kipindupindu katika hospitali ya mji mrara wilayani babati mkoani manyara  wameruhusiwa  baada ya kupatiwa matibabu ambapo wananchi wametakiwa kuendelea  kuchukua taadhari ya  kujikinga na ugonjwa huo kwa kuwa na vyoo bora.

hayo yamebainishwa na Afisa afya Halimashauri ya  mji wa babati Emanuel Kimonge alipokuwa  akiongea na fm manyara, amesema hatua ambazo zimechukuliwa na halimashauri ni pamoja na kuwazuia  mama lishe na baba lishe kupika vyakula pembezoni mwa barabara.

Sauti ya Afisa Afya Emanuel kimonge

kwa upande wake mratibu wa elimu ya afya kwa jamii Halimashauri  ya mji wa Babati Laurencia Urio amesema ugonjwa huo unaenea kutokana na uchafu ambapo   wananachi wanatakiwa kuhakikisha wananawa mikono mara kwa mara. amesema njia nyingine ya kuepukana na ugonjwa huo ni kula chakula cha moto , kufunika chakula, kuosha matunda kabla ya kuyatumia, kuzoa taka zinazozunguka maeneo ya nyumbani, na wanaendelea kutoa elimu hiyo kupitia maeneo mbalimbali yenye mikusanyiko pamoja na katika vyombo vya habari.

Sauti ya mratibu wa elimu ya afya Laurencia Urio.