FM Manyara
FM Manyara
3 April 2026, 12:26

Maafisa wa jeshi la polisi wilayani Babati mkoani Manyara wamepatiwa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia majiko ya kisasa yanayotumia umeme, ikiwa ni juhudi za serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kuendelea kulinda mazingira.
Na Emmy Peter
Elimu hiyo imetolewa na afisa uhusiano kwa umma Tanesco mkoa wa Manyara, Samwel Mandari katika ukumbi wa Polisi messi uliopo Babati, ambapo, amesema matumizi ya majiko ya umeme ni nafuu, yanaokoa muda na gharama, pamoja na kuwa salama kwa mtumiaji.
Mandari amesema majiko hayo ya kisasa aina ya pressure cooker kutoka kwa wakala Sescom, yamethibitishwa na kampuni ya Sescom, yana uwezo wa kuandaa chakula kwa muda mfupi, na kusaidia kuongeza ufanisi katika matumizi ya nishati.
Aidha,amesema maafisa hao wanapaswa kuwa mabalozi wa elimu hiyo kwa jamii, kwa kuwa matumizi ya nishati safi ni sehemu ya mkakati wa serikali katika kulinda mazingi kwa jamii.