FM Manyara
FM Manyara
3 April 2026, 10:44

Zaidi ya wananchi 2700 wamenufaika na kambi ya matibabu ya afya ya siku sita iliyoratibiwa na shirika la SO THEY CAN Tanzania kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya ya Babati mkoani Manyara.
Na Marino Kawishe
Akihitimisha kambi hiyo ya matibabu ya afya iliyofanyika kwenye kata nne zinazofanya kazi na shirika la STC mkuu wa chuo cha elimu maalumu Patandi, mwalimu Lucian Segesela amesema chuo hicho kitaendelea kutoa ushirikiano pamoja na vifaa vitakavyohitajika ili kusaidia upatikanaji wa afua mbali mbali.
Kwa upande wake meneja mkazi wa shirika la STC Roselyne Mariki amekiri kuwepo na mafanikio makubwa na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali ili kufanya kambi zaidi ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wenye changamoto za kifedha .
Nae muuguzi mkuu wa hospital ya wilaya ya Babati sister Thea Funto ametoa wito kwa wananchi kuhudhuria hospital ili kupata matibabu na sio kusubiria kambi za afya ambazo hufanyika mara chache kwenye maeneo yao.

Aidha,kambi nyingine ya afya imepangwa kufanyika kwenye kata nne za galapo, qash, endakiso na mamire mwanzoni mwa mwezi september ambapo wananchi wameomba kuongezwa kwa huduma ya x- ray ili kusaidia wenye uhitaji kwenye eneo hilo.
