FM Manyara
FM Manyara
1 April 2026, 18:43

Wanawake mkoani manyara wametakiwa kulima kilimo cha ikolojia ambacho hakitumia gharama kubwa ili kumuinua mwanamke kiuchumi na kuepelekea kufanya shuguli zake kwa urahisi.
Na Mzidalfa Zaid
Wito huo umetolewa na mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa mkoa wa Manyara Clara Malle, wakati akiongea na fm Manyara amesema kilimo ikolojia ni kilimo rahisi na cha kumrahisishia mwanamke kufanya shughuli zote kwa pamoja.
Kwa upande wake mwanakituo wa taarifa na maarifa Mamire ambae pia ni diwani wa viti maalum wilaya ya Babati Sesilia Cosmas amewataka wananchi kuwania nafasi mbalimbali za za uongozi au maamuzi.
Nae mwenyekiti wa kituo cha taarifa na maarifa Mamire Magreth Basso, amesema kituo hicho kimekuwa kikipambana na ukatili wa kijinsia.