FM Manyara
FM Manyara
21/03/2026, 20:54

Taasisi ya Chem Chem, na Chair The Love kutoka Nchini Marekani kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Babati wamekabidhi viti mwendo zaidi ya 148 kwa wananchi wenye Mahitaji maalumu kutoka Maeneo mbali mbali ya Halmashauri hiyo.
Akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kukabidhi msaada huo kwa wananchi hao wenye uhitaji maalumu Meneja mahusiano na usimamizi wa Miradi ya maendeleo ya jamii kutoka Chem Chem Napendael Wazoel Amesema Lengo lao nikuisaidia Jamii kupitia uhifadhi ambao umeendelea kuwanufaisha Wananchi ambao wapo pembezoni mwa hifadhi.
Aidha akishukuru kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Jofrey Jaffar amewataka Jamii kuendelea kuunga Mkono Taasisi ambazo zimewekeza kwenye Maeneo yao na ambazo zinaigusa jamii moja kwa moja kupitia misaada inayotolewa.
Nao wananchi wenye uhitaji Maalumu wameishukuru Taasisi ya Chem Chem na washirika wake kwa msaada huo huku wakiomba Taasisi hizo kuendelea kutoa msaada kwa wahitaji ambao bado hawajafikiwa kwa njia moja ama nyingine.