FM Manyara
FM Manyara
19/03/2026, 16:58

Vijana mkoani Manyara wamehimizwa kutoa fikra za kuajiriwa na kuweka mawazo yao katika kujiajiri ili kuweza kurithisha vizazi vyao katika biashara zao.
Na Diana Dionis
Hayo yamesemwa na Afisa biashara mkoani Manyara Ally Salehe Mokiwa katika uzinduzi wa Mgendi MinSupermarket yenye Biashara ya vitu mbalimbali vya nyumbani ambapo amesema vijana waliojiajiri wanaweza kuwarithisha watoto wao biashara zao mbali na wale walioajiriwa
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mgendi Minsupermarket John Mgendi, amesema siri ya mafaniko ni kutokukata tamaa na kuwa na imani katika biashara, huku akiwasihi vijana kutokukata tamaa katika utafutaji wao wa kila siku.