FM Manyara

TAKUKURU Manyara yatoa msaada kwa wenye uhitaji na kufuturisha

19/03/2026, 16:37

Picha ya mkuu wa TAKUKURU akikabidhi zwadi za eid kwa watoto wenye uhitaji

Jamii Mkoani Manyara,  imetakiwa kuendelea  kudumisha matendo mema  baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani  na mfungo wa kwaresma kama wanavyo fanya katika kipindi hiki.

Na Mzidalfa Zaid

Hayo yameelezwa na  Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, aliposhiriki  Iftar maalumu iliyoandaliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Manyara, na kuwakutanisha wadau mbalimbali.

sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Mtatifikolo Kaganda
picha ya Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Mtatifikolo Kaganda

Kwa upande wake mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Manyara Bahati Haule, amesema lengo la kuandaa iftar hiyo ni kuiweka TAKUKURU karibu na jamii huku akisema kuwa wametoa msaada kwa watoto yatima katika kituo Cha Hossana home care foundation ambao pia wameshiriki iftar hiyo.

sauti ya mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Manyara Bahati Haule
Picha ya mlkuu wa TAKUKURU mkoa wa Manyara Bahati Haule

Akiongea kwa niaba ya shekhe wa mkoa wa Manyara , Shekhe Ahamad Said ameishukuru TAKUKURU kwa kuandaa iftar hiyo na kuzitaka taasisi zingine kuiga mfano huo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kituo Cha Hossana home care foundation Neema Munisi pamoja na watoto yatima wa kituo hicho  wameishukuru TAKUKURU kwa msaada huo ambao wameutoa.

sauti ya mkurugenzi wa kituo Cha Hossana home care foundation Neema Munisi pamoja na watoto yatima wa kituo hicho