FM Manyara
FM Manyara
10/03/2026, 16:58

Mkoa wa Manyara unatarajia kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno duniani ,ambapo maadhimisho hayo yataadhimishwa kwa kutoa matibabu ya bila malipo ya kinywa na meno kwa wananchi kuanzia march 14 hadi march 18 mwaka huu.
Na Mzidalfa Zaid
Akiongea na fm Manyara msimamizi wa huduma za kinywa na meno Pastory Mahendeka , amesema maadhimisho hayo yatakuwa na huduma mbali mbali ikiwemo elimu ya afya ya kinywa na meno, uchunguzi, matibabu pamoja na mafunzo endelevu kwa wataalamu………….
Kwa upande wake daktari mfawidhi kutoka kitengo cha kinywa na meno hospital ya rufaa mkoa wa manyara Athuman Yatera amesema madaktari bingwa kutoka nchi nzima watakuwepo mkoani manyara ambapo amewataka wananchi wenye changamoto ya kinywa na meno kufika hospital ya mkoa au hospital ya halmashauri kupatiwa matibabu bure.

Nae Mratibu wa kinywa na meno halmashauri ya mji wa Babati Catherine Cuthbert amesema matibabu hayo ya bila malipo yatajumuisha wagonjwa waliotoboka meno , changamoto ya fizi, mpangilio mbaya wa meno na changamoto yeyote ya kinywa na meno.
