FM Manyara

Wananchi Manyara watakiwa kuchukua taadhari dhidi  ya covid 19

05/03/2026, 18:03

picha ya Mganga mkuu wa mkoa wa Manyara Andrew method

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kuchukua taadhari ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo ugonjwa wa covid 19 ambao uliripotiwa hivi karibuni katika baadhi ya maeneo hapa nchini.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa na Mganga mkuu wa mkoa wa Manyara Andrew method , amesema katika kipindi hiki Cha mvua kumekuwa kukitokea magonjwa mengi hivyo wananchi wajilinde wasipate magonjwa hayo ambapo amesema katika mkoa wa Manyara Bado hakujaripotiwa kisa chochote.

Sauti ya Mganga mkuu wa mkoa wa Manyara Andrew method

Kwa upande wake afisa afya mkoa wa Manyara Switen Mwabulambo , amewataka wananchi mkoani Manyara kuzingatia taratibu zote za usafi mara kwa mara ili kuepuka ugonjwa huo.

sauti ya afisa afya mkoa wa Manyara Switen Mwabulambo
picha ya afisa afya mkoa wa Manyara Switen Mwabulambo