FM Manyara

Halmashauri ya mji wa Babati yapanda miti kuelekea siku ya wanawake duniani

05/03/2026, 17:46

Picha ya baadhi ya washiriki wa zoezi la upandaji miti

Katika kuelekea siku ya wanawake Duniani ,Wanawake wa halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara wamepanda miti katika kituo Cha afya Sigino ili kuendelea kutunza mazingira.

Na Mzidalfa Zaid

Afisa maendeleo ambae pia ni mratibu wa dawati la mtambuka kutoka halmashauri  ya mji wa Babati Ivetha Kaoga  amesema kuelekea siku hiyo wamefanya matukio mbalimbali ya kijamii.

sauti ya Afisa maendeleo ambae pia ni mratibu wa dawati la mtambuka kutoka halmashauri  ya mji wa Babati Ivetha Kaoga

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa kituo Cha afya Sigino Joseline Samwel pamoja na mwenyekiti wa kijiji Cha singu Fabian Kombe wamewashukuru wanawake hao kwa kupanda miti katika kituo hicho itakayosaidia wagonjwa kupata kivuli.

Sauti ya mganga mfawidhi wa kituo Cha afya Sigino Joseline Samwel pamoja na mwenyekiti wa kijiji Cha singu Fabian Kombe

Mgeni rasmi katika zoezi hilo alikuwa ni mwenyekiti wa umoja wa wanawake wilaya ya Babati mjini  Eva luoga amewataka Wanawake kuendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali.

sauti ya Mgeni rasmi mwenyekiti wa umoja wa wanawake wilaya ya Babati mjini  Eva luoga
picha ya Mgeni rasmi mwenyekiti wa umoja wa wanawake wilaya ya Babati mjini  Eva luoga
picha ya mmoja wa wanawake walioshiriki upandaji miti