FM Manyara

RC Sendiga akabidhi vyombo vya utoaji huduma ya maji ngazi ya jamii

04/03/2026, 16:33

Picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga akikabidhi vyombo vya Vyombo vya utoaji huduma ya maji ngazi ya jamii (SBWSO)

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amekabidhi Vyombo vya utoaji huduma ya maji ngazi ya jamii (SBWSO) vitakavyosaidia kurahishisha kufikisha huduma ya maji vijijini.

Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza baada ya kukabidhi vyombo hivyo , Sendiga amesema ni jitihada za Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Samia suluhu Hassan katika kufikisha huduma ya maji vijijini ambapo amewataka watumiaji  wa vyombo hivyo kuhakikisha wanavitunza.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga
picha ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Kwa upande wake Meneja wa Ruwasa mkoa wa Manyara James Kionaumela amesema hali ya upatikanaji wa maji katika mkoa wa Manyara ni asilimia 78.09  Hadi  December 2025.

Sauti ya Meneja wa Ruwasa mkoa wa Manyara James Kionaumela
picha ya Meneja wa Ruwasa mkoa wa Manyara James Kionaumela

Baadhi ya watumiaji vyombo hivyo ambao wamekabidhiwa pikipiki, wamesema zitawarahisisha kuyafikia maeneno mengi kwa wakati na kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa wakati.

Sauti ya watumiaji vyombo