FM Manyara
FM Manyara
23 February 2026, 10:26 pm

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga amewaagiza Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini(TARURA) na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD) Mkoa wa Manyara kuomba fedha za dharura katika kipindi hiki cha mvua ili kukarabati barabara zinazoharibiwa na mvua.
Na Mzidalfa Zaid
Amesema hayo Leo katika kikao Cha bodi ya barabara bara mkoa wa Manyara kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara, amesema amepata taarifa ya baadhi ya barabara ambazo zimeharibiwa na mvua ikiwemo barabara ya Bashnet-Orbesh.

Kwa upande wake meneja wa wakala ya barabara (TANROAD) mkoa wa Manyara Dutu masele , amesema changamoto ya mashimo katika bara bara ya Katesh – Singida imesababishwa na magari ya mizigo mizito kuongezeka ambapo kwa Sasa magari 650 hupita mkoani Manyara hali inayopelekea barabara kushindwa kuhimili ambapo changamoto hiyo imefikishwa kwa mtendaji mkuu wa TANROAD.

Aidha meneja wakala ya barabara za vijijini na mijini (TARURA) mkoa wa Manyara Injinia Salim Bwaya amesema wanaendelea kukarabati barabara za mkoa wa Manyara ikiwemo barabara ya kutoka Babati kuelekea ikulu.

