FM Manyara
FM Manyara
17 February 2026, 5:44 pm

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Babati limejadili rasmi ya mpango na bajeti kwa mwaka fedha 2026/2027 na kugusa sekta mbali mbali.
Na Mzidalfa Zaid
Katika baraza hilo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Babati John Noya amewataka madiwani kuhakikisha wanasimamia miradi iliyoko kwenye kata zao kwa kuwa ni wawakilishi wa wananchi.
Noya amesema bajeti ya vituo vyote vya afya katika halmashauri ya wilaya ya Babati ni zaidi ya shilini millioni 655.
kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Babati Anna Mbogo amewataka madiwani kufanya uhamasishaji wa makusanyo ya mapato ya ndani.
Awali baadhi ya madiwani wamelalamikia changamoto ya magari kutopita maeneo ya stendi ikiwemo stendi ya Dareda na kupelekea kupoteza mapato ya ndani.
