FM Manyara
FM Manyara
7 February 2026, 11:01 am

Zaidi kaya maskini 60 katika kijiji cha Imbilili wameanza kunufaika na mpango wa bima wa afya kwa wote katika mpango wa kwanza wa ugawaji wa bima hizo.
Na Emmy Peter
Akikabidhi kadi hizo kwa wananchi hao mkuu wa mkoa wa Mnyara Queen Sendiga amesema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa hadi za Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr.Samia Suluhu Hasani katika siku 100 za uongozi wake ambapo amesema kila mwananchi anatakiwa kupata bima ya afya na katika mkoa wa Manyara zoezi hilo linaendelea kuwafikia wananchi katika maeneo yao.
Aidha mwenyekiti wa kijiji cha Imbilili Marisel Visent ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwakumbuka wananchi wa kaya masikini ambapo amesema ni msaada mkubwa kwa wananchi hao
Sambamba na hilo amewataka wananchi kuendelea kutunza bima hizo ili kuwanufaisha katika matibabu.
