FM Manyara
FM Manyara
6 February 2026, 4:57 pm

Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 267 vya mkoa wa Manyara kwa gharama ya shilingi bilioni 45.8 kupitia wakala wa nishati vijijini (REA).
Na Mzidalfa Zaid
Akizungumza wakati wa kumtambulisha mkandarasi, mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina, amesema mkataba wa utekelezaji mradi huo ni wa miaka 3 katika halmashauri zote za mkoa wa Manyara.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga, amewaagiza wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Manyara kutoa ushirikiano kwa mkandarasi huyo na kutoa elimu kwa wananchi kuwa mradio huo hauna fidia.
Aidha, mkandarasi mkandarasi ambae amekabidhiwa mradi huo Patrick Mong, amesema Wana Lengo la kukamilisha mradi huo kwa miezi 33 na wanaanza kazi February 9 mwaka huu.
