FM Manyara

Mamia wanufaika na kambi ya madaktari bingwa Manyara

26 January 2026, 10:31 pm

Picha ya baadhi ya wanufaika wa Kambi ya Madaktari bingwa Manyara

Mamia ya wananchi wamejitokeza kupata huduma ya mifupa,pua sikio,koo na macho katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Manyara .

Na Mzidalfa Zaid

Hatua hii imekuja baada ya  Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na hospital ya rufaa Kanda ya Mbeya pamoja na Shirika la KCCO kuandaa kambi ya madaktari bingwa maalumu wa mifupa ,pua, sikio,koo na macho ambayo imeanza  Leo January 26 Hadi January 30 mwaka huu wa  kwa lengo la kuwapatia Wateja huduma za kibingwa.

Baadhi ya wagonjwa ambao wamejitokeza kupatiwa matibabu wamesema wamepata huduma nzuri ya matibabu ambapo  wameipongeza hatua hiyo kwani walikuwa wakifuata huduma hizo mbali na kuingia gharama kubwa.

Sauti ya baadhi ya wagonjwa

Kwa upande wake kaimu mganga mfawidhi hospital ya rufaa mkoa wa Manyara Dokta Yesige Mutajwaa Amesema kwa siku ya Leo ya kwanza Zaidi ya wagonjwa 200 wamefika kupatiwa matibabu.

Sauti ya kaimu mganga mfawidhi hospital ya rufaa mkoa wa Manyara Dokta Yesige Mutajwaa
picja ya kaimu mganga mfawidhi hospital ya rufaa mkoa wa Manyara Dokta Yesige Mutajwaa

Nae daktari bingwa wa mifupa  kutoka hospital ya rufaa Kanda ya Mbeya Dokta Baraka Mponda amesema kwa siku ya Leo wamewahudumia wananachi wengi wenye matatizo ya mifupa .

Sauti ya daktari bingwa wa mifupa  kutoka hospital ya rufaa Kanda ya Mbeya Dokta Baraka Mponda

Meneja mradi wa shirika la KCCO Manyara Patricia Malley ambao wamedhamini kambi hiyo, wamesema Lengo la kudhamini ni kuhakikisha wananachi wanapatiwa matiababu ya uhakika.

Sauti ya Meneja mradi wa shirika la KCCO Manyara Patricia Malley