FM Manyara

Kambi ya madaktari bingwa kuanza Januari 26 Manyara

22 January 2026, 7:10 pm

Picha ya wataalam wa afya kutoka hospitali ya Rufaa mkoa wa Manyara

Wizara ya afya chini ya Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na hospital ya rufaa Kanda ya Mbeya pamoja na shirika la KCCO wameandaa kambi ya madaktari bingwa maalumu wa mifupa ,pua, sikio,koo na macho itakayofanyika mkoani Manyara kuanzia January 26 mpaka 30 mwaka huu wa 2026 kwa lengo lakuwapatia Wateja huduma za kibingwa.

Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza na Fm Manyara Afisa muuguzi msaidizi  kutoka Kitengo cha Macho hospitali ya Rufaa mkoa wa Manyara Faraja Mapunda amesema huduma zitakazotolewa ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya mifupa, pua, sikio,koo,macho

sauti ya Afisa muuguzi msaidizi  kutoka Kitengo cha macho Faraja Mapunda
Picha ya Afisa muuguzi msaidizi  kutoka Kitengo cha Magonjwa ya ndani Faraja Mapunda

Kwa upande wake Afisa Muuguzi msaidizi kutoka hospitali ya Rufaa mkoa wa Manyara Macrina Kilamba ameelezea faida za kambi hiyo ya siku tano na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupima afya zao.

Sauti ya afisa Muuguzi msaidizi kutoka hospitali ya Rufaa mkoa wa Manyara Macrina Kilamba
picha ya afisa Muuguzi msaidizi kutoka hospitali ya Rufaa mkoa wa Manyara Macrina Kilamba