FM Manyara

Sekta za Maji Manyara, zakutana kujadili upatikanaji wa maji kwa asilimia 99

16 January 2026, 9:00 pm

Picha ya Baadhi ya viongozi wa sekta ya maji Manyara

Mamlaka za maji ikiwemo Ruwasa, Bawasa na waatalam kutoka Maabara za maji mkoa wa Manyara na bonde la maj na bonde la kati zimekutana kwa pamoja na kuunda timu kwa ajili ya kuweka mipango ya upatikanaji wa maji ili ifikapo mwaka 2030 mkoa wa Manyara unakuwa na maji kwa asilimia 99.

Na Mzidalfa Zaid

Akiongea baada ya kikao hicho Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Babati(BAWASA) Iddi Msuya amesema wameweka mkakati wa kuhakikisha wanashirikiana kufanikisha upatikanaji wa maji mjini na vijijini.

Sauti ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Babati(BAWASA) Iddi Msuya

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya maji na usafi wa mazingira vijijini(RUWASA) Injinia James Kionaumela, amesema mashirikiano hayo yatasaidia kupunguza changamoto mbalimbali ikiwemo kuazimana vifaa.

Mkuu wa Maabara ya maji mkoa wa Manyara Nikolaus Germanus, amesema hali ya ubora wa maji katika mkoa wa Manyara inaridhisha.

Sauti ya Mkuu wa Maabara ya maji mkoa wa Manyara Nikolaus Germanus

Nae Mhandisi wa maji kutoka Bonde la maji, bonde la  kati katika ofisi ya Babati  Denis Gunze, amesema wameweka mikakati ya kuhakisha wanafanya utafiti juu ya upatikanaji wa maji sehemu yenye maji.

Sauti ya Mhandisi wa maji kutoka Bonde la maji, bonde la  kati katika ofisi ya Babati  Denis Gunze