FM Manyara

RC Sendiga awataka wazazi kuwapeleka shule wanafunzi ambao hawajaripoti shule

16 January 2026, 9:03 pm

Picha ya Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga

Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga amewataka wazazi na walezi mkoani Manyara kuhakikisha wanawapeleka shule watoto ambao wanatakiwa kwenda shule kwakuwa  bado wapo wanafunzi ambao  hawajaripoti.

Na Mzidalfa Zaid

Amesema hayo leo  wakati akiongea na waandishi wa habari ofisni kwake, amesema mpaka sasa wanafunzi wachache wa kidato cha kwanza wameripoti hivyo  viongozi wa kata na vijiji wanaendelea na misako ya kuwatafuta wanafunzi ambao hawajaripoti.

sauti ya Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga

Aidha, amewataka wazazi na walezi mkoani hapa  kuchangia chakula mashuleni ili watoto wapate haki yao ya msingi ya kupata lishe bora na masomo.