FM Manyara

TMDA yawataka wananchi kuhifadhi, kutumia dawa kwa usahihi

13 January 2026, 7:01 pm

Picha ya na Meneja wa  Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA Kanda ya kaskazini Proches Patrick

Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA Kanda ya kaskazini imetoa elimu kwa wananchi mkoani Manyara na kanda ya kaskazini kwa ujumla namna ya kuhifadhi dawa ili zisipoteza uwezo wa kufanya kazi.

Na Mzidalfa Zaid

Elimu hiyo imetolewa na Meneja wa  Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA Kanda ya kaskazini Proches Patrick wakati akiongea na fm Manyara, amesema dawa hazipaswi kuhifadhiwa sehemu ambayo ina maji, au joto  kali.

Sauti ya Meneja wa  Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA Kanda ya kaskazini Proches Patrick

Aidha, amewataka wananchi wa Kanda ya kaskazini kwa ujumla kuzingatia matumizi sahihi ya dawa kama wanavyoshauriwa na daktari.