FM Manyara

Khambay aahidi kukuza elimu Babati Mji

8 January 2026, 7:39 pm

Picha ya Mbunge wa jimbo la Babati Mjini Mhe Emmanuel Khambay

Mbunge wa jimbo la Babati Mjini Mhe Emmanuel Khambay amehaidi kusaidia wananchi wa jimbo hilo kupata Kituo cha kudurufu mitihani ya majaribio kwa wanafunzi wanaosoma sekondari ili kupandisha ufaulu wao kwa shule za serikali zilizopo jimboni kwake.

Na Marino Kawishe

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Nangara, amesema mpango huo utakuwa ni wakuboresha eneo la ufaulu kwa wanafunzi ili waendenane na shule za binafsi ambazo zimekuwa zikifanya vizuri ambapo ameshauri mitihani hiyo iwe inafanyika kila mwezi.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Babati Mjini Mhe Emmanuel Khambay

Kwenye ziara hiyo Mh Khambay  ameambatana na baadhi ya  wataalamu kutoka ofisi ya halmashauri ya mji wa Babati  waliojibu kero zilizoulizwa na wananchi moja kwa moja huku akiwata kuendelea kushirikiana na wananchi kuleta maendelo na  kuacha kusuasua na kuwapatia wananchi huduma wanazostahili bila upendeleo.