FM Manyara

Serikali kuwabana wazazi wasiotimiza wajibu wao

7 January 2026, 5:17 pm

Picha ya Mkuu wa mkoa wa Manyara  Queen Sendiga

Mkuu wa mkoa wa Manyara  Queen Sendiga, amewataka wazazi na walezi mkoani Manyara  kuhakikisha wanawapeleka watoto shule mwanzoni mwa mwaka  huu wa masomo  nakusema  wazazi wanapaswa kutoa  ushirikiano  kwa walimu  kuhusu utoaji wa chakula mashuleni.

Na Emmy Peter

Sendiga ameyasema   hayo katika kijiji cha Chem chem kata ya Mutuka  ambapo amewataka makatibu Tawala, na Watendaji wa kata  hiyo pamoja  na maafisa elimu kata kuhakikisha malengo ya mkoa yaliyowekwa yanatimia  kwa kuhakikisha wanafunzi wanaingia shule kwa wakati.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Manyara  Queen Sendiga

Aidha, Sendiga  amesema serikali itaandaa sheria zitakazowabana wazazi wasiotimiza wajibu huo kwa  watoto wao kuwapeleka shule kwakua  ni maelekezo ya serikali.