FM Manyara

Serikali Manyara yawataka wananchi kutovamia maeneo ya wazi

7 January 2026, 4:48 pm

Picha ya Kamishna wa ardhi mkoa wa Manyara Wensilaus Mtui

Serikali mkoani Manyara imewataka wananachi mkoani Manyara  kutovamia maeneo yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya shughuli maalum ili kuepuka migogoro ambayo imekuwa ikitokea.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa leo na Kamishna wa ardhi mkoa wa Manyara Wensilaus Mtui wakati akiongea na fm Manyara, amewaonya wananachi wenye tabia hiyo ya kuvamia maeneo ya serikali na kufanya shughuli zao za kiuchumi.

Aidha,amewataka wananachi kufuata  sheria za umiliki wa ardhi kwa kuhakikisha maeneno yao yanapimwa  na kumilikiwa  ili kusitokee mgongano wa kiwanja kimoja kumilikiwa na watu zaidi ya mmoja .