FM Manyara

TMA Manyara yatoa mwelekeo wa mvua mwezi Januari

5 January 2026, 5:28 pm

picha ya Meneja wa mamlaka ya hali ya hewa mkoa wa Manyara Salma Amour

Wananchi  mkoani Manyara  wameshauriwa  kuendelea kufuatilia  ushauri unaotolewa na Mamlaka hiyo ili kuwasaidia katika shughuli zao.

Na Mzidalfa Zaid

Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa mkoa wa Manyara Salma Amour ameyasema hayo leo wakati akiongea na FM Manyara, amesema  kwa mwezi Januari vipindi  vya mvua  vinatarajiwa katika maeneo machache ambapo amesema kuanzia Januari 5 hadi 10 vipindi vya mvua chache vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Manyara.

Sauti ya Meneja wa TMA Mkoa wa Manyara Salma Amour

Aidha, amewashauri wakulima, wafugaji pamoja na wavuvi  kufuatilia utabiri unaotolewa na TMA ili kurahisisha shughuli zao zao kila siku.