FM Manyara

NSSF Manyara yawataka waajiri kulipa michango kwa wakati

22 December 2025, 9:22 pm

Picha ya Meneja wa NSSF mkoa wa Manyara Alexanda Joseph

Waajiri mkoani Manyara wametakiwa kulipa michango ya wafanyakazi  kwa wakati pamoja na kuwaandikisha wafanyakazi wote ambao hawajandikishwa katika mfuko wa Taifa wa hifadhi ya jamii(NSSF) ili wanufaike na fursa mbalimbali zinazopatikana katika mfuko huo.

Na Mzidalfa Zaid

Hayo yameelezwa leo na Meneja wa NSSF mkoa wa Manyara Alexanda Joseph wakati akiongea na fm Manyara, amesema kumekuwepo na changamoto ya baadhi ya waajiri ambao wamekuwa wakilipa michango midogo tofauti na mishahara ambayo wafanyakazi wanapokea, ambapo amekemea vitendo hivyo.

Sauti ya Meneja wa NSSF mkoa wa Manyara Alexanda Joseph

Aidha, amewataka wafanyakazi wote ambao wamekuwa wakifanya kazi bili kupeleka  michango NSSF wafike kwenye ofisi za NSSF Manyara ili hatua zaidi za kisheria zichukuliwe na wafanyakazi hao wapate haki zao.