FM Manyara

RC Sendiga azindua bima ya afya kwa wote Manyara

19 December 2025, 7:37 pm

Picha ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Mpango wa uhamasishaji  wa Bima ya afya kwa wote umezinduliwa katika katika mkoa wa Manyara  utakao saidia wananchi wa mkoa wa Manyara kupata huduma za matibabu kwa urahisi na unafuu.

Na Emmy Peter

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga  amezindua  mpango wa uhamasishaji  wa utekelezaji  wa Bima ya afya kwa wote ambapo mpango huo umezinduliwa katika halmashauri ya mji wa Babati na utasaidia kupunguza gharama  za matibabu kwa wananchi  wa mkoa wa Manyara..

Sendiga amezindua mpango huo leo katika ukumbi wa  chuo kikuu Huria mjini Babati,  amesema mpango huo wa Bima ya afya NHIF kwa wote  utasaidia wananchi wa mkoa wa Manyara kupata huduma za matibabu kwa urahisi na unafuuu  na wananchi  watapatiwa elimu kuhusu umuhimu wa Bima ya afya  kwa mtu mmoja  mmoja  itakayosaidia katika matibabu.

sauti ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Kwa upande wake mganga mkuu wa  mkoa wa Manyara  Dokta Andrew Method amesema  kwa mkoa wa Manyara imekuwa  ni fursa katika kuendelea  kuboresha huduma  za afya kwa wananchi katika Halmashauri zote 7 ndani ya mkoa wa Manyara na wamejipanga kupeleka  elimu hiyo katika makundi mbali mbali.

sauti ya mganga mkuu wa  mkoa wa Manyara  Dokta Andrew Method

Aidha watumishi wa afya  wa mkoa wa Manyara wameishukuru serikali ya awamu ya sita  kuleta huduma hiyo  ya Bima ya afya kwa wote  kwakua  itasaidia kuleta  unafu katika kazi zao na kuondoka na msamahaa wa wagonjwa wanao shindwa kulipia huduma hizo za matibabu.

sauti ya watumishi wa afya  wa mkoa wa Manyara