FM Manyara

Milion 156 zakamilisha zahanati ya Endagile-Manyara

19 December 2025, 10:14 am

picha ya zahanati ya Endagile

Zaidi ya shilingi milion 150 zimetumika kukamilisha ujenzi wa zahanati ya Endagile iliyopo kata ya Mamire wilayani Babati mkoani Manyara ambapo wananchi wa kijiji hicho wamechangia fedha na nguvu kazi huku pia wadau na mbunge wa jimbo la Babati vijijini kuchangia kukamilika kwa majengo hayo.

Na Marino Kawishe

Akizungumza mbele ya wananchi wa kijiji hicho mgeni rasmi ambae ni  mkurugenzi wa halmashauri ya wilayani ya Babati Anna Mbogo amesema baada yakukamilika kwa zahanati hiyo inatoa fursa kwa wananchi wa kijiji hicho na jirani kupata matibabu mbali mbali na kuondokana na umbali mrefu uliokuwepo hapo awali.

sauti ya kurugenzi wa halmashauri ya wilayani ya Babati Anna Mbogo
picha ya viongozi mbalimbali akiwemo mkurugenzi wa halmashari ya wilaya ya Babati na Mganga mkuu wa wilaya ya Babati

Kwa upande wake mganga mkuu wa hospital ya wilaya ya Babati Dr Madama Hosea amesema huduma zinaanza kutolewa mara moja baada ya kukamilika kwa majengo ya zahanati hiyo huku akitaja baadhi ya huduma zitakazoanza kutolewa kuanzia dec 19.

sauti ya mganga mkuu wa hospital ya wilaya ya Babati Dr Madama Hosea

Naye mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa mkoani Manyara Clara Malley amesema wao kama wanakikundi mnamo mwaka 2022 walitoa pendekezo kwa mkurugenzi wa halmashauri kujengwa zahanati na miundo mbinu mingine itakayosaidia wananchi hasa wakati wa mvua.

sauti ya mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa mkoani Manyara Clara Malley

Wakionge na Fm Manyara redio  wananchi wa kijiji hicho wamekiri uwepo wa zahanati hiyo , ambapo wamesema itawasaidia kupata huduma ikiwemo clinic kwa wajawazito na huduma nyingine zitakazotolewa na wataalamu wa afya.

sauti ya Wananchi
picha yabaadhi ya wananchi wa kijiji cha Endagile kata ya Mamire