FM Manyara

RC Sendiga azindua Clinik ya madaktari bingwa Mbulu

16 December 2025, 5:47 pm

Picha ya madaktari bingwa

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga  amezindua clinik ya madaktari bingwa ya magonjwa ya binadamu  katika halmashauri ya mji  Mbulu ili kuwasaidia  wananchi kupunguza  kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya za kibingwa

Na Emmy Peter

Sendiga  amezindua kliniki hiyo ikiwa ni  mwendelezo wa ziara yake katika mkoa wa Manyara ambapo  amesema tangu kuanzaa kwa zoezi la huduma hiyo ya clinik za madaktari  bingwa wamesha hudumia zaidi ya wagonjwa  2174 na huduma hiyo imesaidia wananchi  kupata  huduma kwa haraka.

sauti ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga  

Kwa upande  wao wananchi  wameishukuru serikali ya awamu ya 6 kwa kuwasogezea huduma hizo karibu kwakua  huduma hiyo walikuwa wakiifata nje ya  mkoa  wa Manyara.

sauti ya wananchi