FM Manyara

Wananchi Manyara fatilieni taarifa za hali ya hewa-TMA

15 December 2025, 4:46 pm

Picha ya Meneja wa TMA mkoa wa  Manyara Salma Amour

Wananchi mkoani Manyara wameshauriwa  kufuatilia taarifa zinazotolewa na Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA)pamoja na kuwasiliana na maafisa ugani wa maeneo yao ili wajue mbegu zinazofaa kupanda na kulima kwa kuhifadhi maji wakati huu wa msimu wa mvua chache .

Na Mzidalfa Zaid

Hayo yamesemwa na Meneja wa TMA mkoa wa  Manyara Salma Amour alipokuwa akizungumza na fm Manyara amesema kwa mkoa wa Manyara mvua zinatarajiwa kuwa za wastani hadi  chini ya wastani kwa msimu huu wa mvua za mwezi december.

sauti ya Meneja wa TMA mkoa wa  Manyara Salma Amour

Aidha Amour  amewataka wananchi kuchukua tahadhari za mapema ikiwemo kuhifadhi chakula cha kutosha kwaajili ya matumizi yao ya badae pamoja na chakula cha mifugo.