FM Manyara

ACP Mwakabonga  afanya ukaguzi mabasi  ya usiku Manyara

13 December 2025, 11:27 am

Madereva  kote nchini wametakiwa kuacha tabia ya kuendesha vyombo vya Moto pindi wanapotumia vilevi kwakua itasaidia kupunguza ajali  za barabarani msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

Na Emmy Peter

Kamishina msaidizi wa Polisi (ACP) Joseph Mwakabonga  kutoka kikosi cha usalama barabarani nchini  ameyasema hayo alipokuwa katika ziara yake  ya ukaguzi wa mabasi ya safari za usiku mkoani Manyara, amesema wameanza zoezi la ukaguzi wa magari hayo na kubani baadhi ya makosa.

Sauti ya Kamishina msaidizi wa Polisi (ACP) Joseph Mwakabonga  kutoka kikosi cha usalama barabarani nchini

Mwakabonga amesema  Katika kipind hiki Cha sikukuu wamebaini kuna makosa ambayo madereva wanayafanya kwa kuendesha magari kwa mwendo kasi bila kuchukua tahadhari  ambapo amewataka kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

sauti ya Kamishina msaidizi wa Police (ACP) Joseph Mwakabonga  kutoka kikosi cha usalama barabarani nchini

Aidha, Mwakabonga Amesema Katika zoezi hilo la ukaguzi wa magari wamejipanga kuhakikisha madereva wote wanakuwa na leseni na zoezi hilo ni endelevu ambapo linafanyika  usiku na mchana