FM Manyara

Magari ya shule yakaguliwa Manyara

8 December 2025, 5:11 pm

picha ya baadhi ya magari ya shule yakifanyiwa ukaguzi

Wamiliki wa magari ya shule mkoani  Manyara wametakiwa  kusimamia magari ya kubeba wanafunzi  na kuhakikisha magari hayo ni mazima ili kuondokana na ajali zinazo sababishwa na magari mabovu.

Mkuu wa kikosi cha usalama bara barani mkoa wa Manyara Michael Mwakasungula, ameyasema hayo alipokuwa katika zoezi la ukaguzi wa magari ya shule  amesema mwitikio kwa wamiliki wa magari ya shule ni mkubwa  na wanaendelea  kujitokeza kupeleka magari yao kukaguliwa  na kubaini changamoto za magari hayo ya kubebea wanafunzi.

Sauti ya mkuu wa kikosi Michael Mwakasungula

Kwa upande wake mkaguzi wa magari  wilaya ya Babati sajent Mohamed Yahaya amesema katika ukaguzi huo  uliyo fanyika wamekagua ufanyaji wa kazi wa mifumo yote ya magari ya shule na kubaini baadhi ya changamoto katika  magari hayo ambapo wamewataka  wamiliki  kuwa na utaratibu wakupeleka magari hayo kukaguliwa mara kwa mara.

Sauti ya mkaguzi wa magari Sajent Mohamed Yahaya