FM Manyara

Madiwani Babati mji watakiwa kusimamia sheria

2 December 2025, 8:36 pm

picha ya baadhi ya madiwani wa halmashauri ya mji wa Babati

Madiwani  kutoka  kata za halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara wameapishwa  rasmi leo kuanza kutekeleza majukumu yao pamoja na kufanyika  uchaguzi wa kumchangua mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa Baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Babati.

Na Mzidalfa Zaid

Akitangaza matokeo hayo, Katibu tawala wilaya ya Babati Thobias Abwao amesema Yona Wao amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Baraza la madiwani kwa kwa kura zote 12 za wapiga kura na Salome Masasi  ameshinda nafasi ya makamu mwenyekiti kwa kupata kura zote 12 za ndio.

sauti ya Katibu tawala wilaya ya Babati Thobias Abwao amesema Yona Wao

Akizungumza kwa niaba ya ofisi ya mkoa wa Manyara, Afisa elimu ya watu wazima Ibrahim Mbogo , amewataka viongozi hao kutenda haki na kusimamia sheria pamoja na kusimamia ipasavyo ukusanyaji wa mapato.

sauti ya mwakilishi wa ofisi ya mkoa wa Manyara ambae ni Afisa elimu ya watu wazima Ibrahim Mbogo ,

Mwenyekiti wa Baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Babati  Yona Wao amesema atafaata miongozo bila kumuonea mtu, ambapo amewaomba madiwani kumpa ushirikiano.

sauti ya Mwenyekiti wa Baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Babati  Yona Wao

Nae makamu mwenyekiti wa Baraza hilo Salome Masasi , amemshukuru Mungu kwa kuchaguliwa na kusema kuwa atamshauri mwenyekiti katika kuhakikisha kazi zinafanyika vizuri.

Sauti ya makamu mwenyekiti wa Baraza hilo Salome Masasi

Aidha,  Mbunge wa jimbo la Babati mjini Mmmanuel Khambay  amesema atashirikiana na viongozi hao huku akiwataka viongozi hao  wasiwe chanzo cha migogoro badala yake wawe mstari wa mbele kushirikiana katika kuleta maendeleo ya wananchi.

sauti ya Mbunge wa jimbo la Babati mjini Mmmanuel Khambay