FM Manyara

Wakulima Manyara washauriwa kulima kilimo cha kisasa

28 November 2025, 2:02 pm

Picha ya viongozi wa AgroGlobe

Wakulima mkoani Manyara wametakiwa kulima kilimo cha kisasa kwa kutumia mbegu na viuatilifu bora pamoja na kuzingatia ushauri unaotolewa  na wataalamu wa  kilimo katika maeneo yao.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo Umetolewa na  mwakilishi wa  mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Grace Lambau wakati akiongea katika semina ya kilimo  ambayo imeandaliwa na kampuni ya AgroGlobe Limited kwa kushirikiana na kampuni ya Fide mamba Agrovert kwa lengo la kuwaelimisha wakulima kuhusu kilimo bora .

Sauti ya mwakilishi wa  mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Grace Lambau

Akizungumzia lengo la mafunzo hayo afisa mauzo wa kampuni ya Agroglobe limited kanda ya Pwani Alex King amesema wamewakutanisha wakulima hao kwa lengo la kuwapa elimu namna ya kuandaa kilimo bora.

Sauti ya afisa mauzo wa kampuni ya Agroglobe limited kanda ya Pwani Alex King

Nae Meneja wa fide Mamba Agrovert Manka John, amesema mkulima anapaswa kutumia pembejeo bora ili apate mazao mengi na kuwa na uhakika wa kilimo chake.

sauti ya Meneja wa fide Mamba Agrovert Manka John
picha ya Meneja wa fide Mamba Agrovert Manka John

Aidha,baadhi ya wakulima ambao wameshiriki Semina hiyo wamezishukuru kampuni hizo kwa kuwa wamefaham namna ya kuandaa kilimo cha kisasa ambapo wakulima hao wamepata nafasi ya kusajiliwa namba za ruzuku pamoja na kupimiwa udongo.

sauti ya wakulima ambao wameshiriki semina
picha ya baadhi ya wakulima walioshiriki semina