FM Manyara

TGNP yazinoa kamati za viongozi MTAKUWWA

27 November 2025, 4:31 pm

Picha ya mkufunzi kutoka TGNP Deogratius Temba akitoa mafunzo kwa viongozi mbalimbali waliohudhuria warsha ya mafunzo ya ukatili wa kijinsia mjini Babati mkoani Manyara.

Mtandao wa jinsia tanzania (TGNP) imetoa mafunzo kwa kamati za viongozi ngazi ya vijiji na kata

Na Marino Kawishe

Mtandao wa jinsia tanzania (TGNP) umeendesha mafunzo yakuwajengea uwezo viongozi warakibishi waliopo kwenye kamati za mpango wa taifa wakutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto MTAKUWWA kutoka vituo vya taarifa na maarifa wilayani Mbulu na halmashauri ya wilaya ya Babati Mkoani Manyara. 

Akizungumza na fm manyara radio  mkufunzi wa warsha hiyo kutoka mtandao wa jinsia tanzania (TGNP) Deogratias Temba amesema lengo la semina hiyo ni kuwajengea uwezo wawakilishi hao ambao wataenda kuelimisha jamii na kuendeleza mapambano ya ukatili unafanyika kwenye maeneo yao.

Sauti ya mkufunzi kutoka TGNP Deogratius Temba

Kwa upande wake mwakilishi wa washiriki wa warsha hiyo kutoka kata ya mamire Malik Kimaro amesema kumekuwa  na mafanikio makubwa kwenye eneo la mamire na kukiri ukatili unaendelea kupungua kwa sababu ya mafunzo wanayopata mara kwa mara.

Sauti ya mwakilishi wa washiriki kutoka kata ya mamire Malik Kimaro

Warsha hiyo ya siku Tatu kuhusu mpango wa taifa wakutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na Watoto (MTAKUWWA) imeangazia pia masuala ya ustawi wa jamii na ukatili wa kijinsia na jinsi ya kukabiliana na kesi za ukatili pale zinapowasilishwa kwenye kamati za MTAKUWWA.

Picha ya washiriki wakifuatilia mafunzo yaliyotolewa na TGNP