FM Manyara

Tanesco Manyara kuweka Mita Janja

26 November 2025, 12:52 pm

Shirika  la Umeme Tanzania Tanesco mkoa wa Manyara limeanza zoezi la kubadilisha Mita za umeme kwa kuondoa mita za zamani na kufunga mita janja (Smart Meters ) mita ambazo zitawezesha wateja pindi wanaponunua  umeme kuingia moja kwa moja .

Na Mzidalfa Zaid

Afisa uhusiano wa Tanesco mkoa wa Manyara Samwel Mandar ameyasema hayo wakati akiongea na Fm Manyara, amesema zoezi hilo litafanyika nyumba kwa nyumba na zoezi hilo limeanzia wilayani Babati.

Sauti ya afisa uhusiano wa Tanesco mkoa wa Manyara Samwel Mandar

Aidha,amesema katika zoezi hilo salio la unit zinazobakia kwenye mita ya awali zitahamishiwa  kwenye mita mpya inayowekwa na hakutakuwa na malipo yoyote  katika uboreshaji huo.