FM Manyara

MVIWATA-jitokezeni changamoto za ukatili wa kijinsia Manyara

26 November 2025, 12:24 pm

picha ya baadhi ya wanachama wakipata elimu

Kuelekea  siku 16 za kupinga  ukatili wa kijinsia, wakulima wadogo Mkoa wa Manyara wametakiwa  kujitokeza katika Madawati ya kisheria  ili  kupeleka changamoto za ukatili wanazo kutananazo.

Na Emmy Peter

Hayo yamesemwa leo  na  Mhandisi Agrey Mahole ambae amemuwakilisha mkuu wa wilya ya Babati  katika ofisi za chama cha wakulima wadogo MVIWATA  zilizopo   wilayani   Babati Mkoani  Manyara  Amesema wakulima wadogo wamekuwa wakipata changamoto hizo ya ukatili huo katika Maeneo hayo

sauti ya Mhandisi Agrey Mahole

Aidha Mratibu wa Mviwata Malkiadi Maega  kutoka Tawi la Manyara Amesema wamefanya Mkutano na wananchama wa chama hicho   kuelekea katika maadhimisho hayo kupinga   siku 16 za ukatili wa kijinsi Ambapo amesema ukatili unaomgusa Mkulima Mdogo Ni tofauti na ukatili wa Mjini kwakuwa  Inachangia kumkandamiza Mwanamkeee kiuchumi.

Sauti ya Mratibu wa Mviwata Malkiadi Maega

Kwa upande  wao wanachama wa chama hicho wamemshukuru mkuu wa wilaya ya Babati kwa kuendea kuunga mkono juhudi za wanawake kiuchumi na kupeleka elimu vijijini na katika mabaraza la wazee ili kukemea ukatili huo.

sauti ya wanachama