FM Manyara

DCEA na TAKUKURU zashirikiana kutoa elimu ya kupambana na dawa za kulevya vyuoni

19 November 2025, 12:17 pm

Picha ya Afisa elimu jamii kutoka Mamalaka ya kudhbiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini Shaban Miraji

Wanafunzi wa vyuo vya kati na vyuo vikuu mkoani Manyara wametakiwa kuacha  kujiingiza katika makundi yasiyofaa ya kujihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya kwakua  itachangia  kushuka  kwa elimu na kupoteza nguvu kazi ya Taifa.

Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza na Fm Manyara, afisa ustawi wa jamii kutoka Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini Sara Ndaba amesema  wanaendelea kutoa elimu katika vyuo vya kati na vyuo vikuu ndani ya mkoa wa Manyara katika kupambana  na matumizi ya dawa za kulevya.

Sauti ya Afisa ustawi wa jamii kutoka Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini  Sara Ndaba

 Ndaba amesema lengo la kufikisha elimu hiyo vyuoni  ni kuwafahamisha madhara ya matumizi ya dawa za kulevya ambapo amesema kuna baadhi ya wananafunzi wamejiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya  na kushindwa kufikia malengo yao.

Picha ya afisa ustawi wa jamii kutoka Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya  Sara Ndaba

Kwa upande wake afisa elimu jamii kutoka Mamalaka ya kudhbiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini Shaban Miraji, amesema  mtu anapo jihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya anaweza kufanya vitendo visivyofaa  na kujishushia  utu wake  ikiwemo uporaji  au ugomvi.

sauti ya afisa elimu jamii kutoka Mamalaka ya kudhbiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini Shaban Miraji
picha ya afisa elimu jamii kutoka Mamalaka ya kudhbiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kaskazini Shaban Miraji

Afisa TAKUKURU  mkoa wa Manyara Mwinyi Hamisi amesema TAKUKURU wana utaratibu wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuanzia ngazi ya msingi hadi vyuoni ili waweze kuwasaidia kutoa taarifa pamoja na elimu dhidi ya rushwa na matumizi ya dawa za kulevya.

sauti ya Afisa TAKUKURU  mkoa wa Manyara Mwinyi Hamisi