FM Manyara

DC Kaganda awataka wananchi kutunza vyanzo vya maji

15 November 2025, 11:44 am

Picha ya mkuu wa wilaya akiwa na wataalam mbalimbali wakati akikagua mradi wa Maji

Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda amewataka wananchi wilayani Babati mkoani Manyara kutunza vyanzo vya maji ikiwemo kutofanya shughuli zao karibu na vyanzo hivyo.

Na Mzidalfa Zaid

Kaganda amesema hayo baada ya kukagua miradi ya maji ukiwemo mradi wa Darakuta na mradi wa chanzo cha maji Mrara, ambapo  amewataka wananchi kuendelea kutunza vyanzo hivyo ikiwemo kutokata miti hovyo.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Amesema mradi wa chanzo cha maji Darakuta utanufaisha wananchi zaidi ya elfu30 na mradi wa chanzo cha maji Mrara utanufaisha wananchi zaidi ya elfu 20.

sauti ya Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Babati(BAWASA) Iddi Msuya, amesema kata ya Nkaiti ni miongoni mwa kata ambayo itanufaika na mradi wa Darakuta.

Sauti ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Babati(BAWASA) Iddi Msuya

Nao baadhi ya wananchi wa wilaya ya Babati ambao wanatarajia kunufaika na mradi huo, wamesema kutokana na changamoto ya maji waliyonayo, miradi hiyo itasaidia kutatua changamoto hiyo ya maji.

sauti ya wananchi