FM Manyara

DC Babati azindua kampeni ya matumizi ya nishati safi  na kugawa majiko banifu

13 November 2025, 11:00 am

Picha ya mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda akikabidhi majiko kwa makundi maalum

Mkuu wa wilaya ya Babati mkoani Manyara Emmanuela Kaganda, amezindua kampeini ya nishati safi na kuhamasiha matumizi ya majiko salama kwa mazingira katika wilaya hiyo.

Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza katika uzinduzi huo, Kaganda amesema kampeini hii itasaidia kutokomeza nishati chafu,kwani  serikali imetenga fedha nyingi  kwa kuandaa nishati safi ili kuwasaidia wananchi wa vijijini katika shughuli zao.

sauti ya Mkuu wa wilaya ya Babati mkoani Manyara Emmanuela Kaganda

Kwa upande wake mhandisi wa miradi REA  Ramadhani Mganga, amesema Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan, ametenga jumla ya shilingi bilioni 9 kuhakikisha kila mwananchi anatumia nishati safi na mkoa wa Manyara umepatiwa majiko zaidi ya 7000.

sauti ya mhandisi wa miradi REA  Ramadhani Mganga

Mwakilishi wa kampuni ya LS SOLUTION LIMITED  amesema majiko hayo yanatumia kuni kidogo hivyo yatasadia kupunguza gharama kubwa  za matumizi ya kupikia.

sauti ya Mwakilishi wa kampuni ya LS SOLUTION LIMITED

Aidha  baadhi ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya ya Babati, ambao wamejitokeza kununua majiko hayo ya bei nafuu, wameishukuru serikali kwa kugharamia asilimia 80 ya bei ya majiko hayo .

picha ya baadhi ya wananchi waliojitokeza katika kata ya Magugu kununua majiko ya bei nafuu