FM Manyara

Zaidi ya shilingi bil 2 zatekeleza miradi mbalimbali Gidas

18 October 2025, 9:00 pm

Picha ya mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM Daniel Baran Sillo akinadi sera na ilani ya chama chake kwa wananchi wa kata ya Gidas wilayani Babati Mkoani Manyara

Na Marino Kawishe

Zaidi ya shilingi Bilion mbili  zimetekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika kata ya Gidas chini ya uongozi wa Mbunge wa jimbo la Babati Vijijini kwa kipindi cha miaka minne iliyopita wakati huu wa uongozi wa Rais Samia Suluhu.

 Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa Hadhara wa kampeni  kunadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM Daniel Baran Sillo amesema bado Kuna changamoto chache zilizosalia ambazo akipata Ridhaa ya kuchaguliwa Katika uchaguzi utakaofanyika October 29 atazikamilisha kwa kipindi cha miaka mitano.

Sauti ya mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM Daniel Baran Sillo

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Babati Vijijini Jackson Haibey amewata wananchi kujitokeza kupiga kura kwani ni haki yao kikatiba kumchagua Rais, Mbunge na Diwani katika uchaguzi mkuu utakaofanyika October 29 mwaka huu.

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Babati Vijijini Jackson Haibey
Wananchi wa kata ya Gidas wakisikiliza sera na ilani za Chama Cha Mapinduzi katika mkutano wa kampeni wa mgombea ubunge Jimbo la Babati vijijini Daniel Sillo