FM Manyara

Wananchi zaidi ya laki moja kunufaika na mradi wa maji Mbulu

18 July 2025, 4:57 pm

picha ya tenki la maji

Mwenge wa uhuru umezindua mradi wa  tenk la kuhifadhia  maji lenye ujazo wa lita million mbilis  lenye thamani ya zaidi ya shilingi billion 41 katika wilaya ya Mbulu kwakua  itasaidia kuondokana na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama kwa wananchi  katika kijiji hicho.

Na Emmy Peter

Akizungumza  baada ya kuzindua mradi huo kutoka wakala wa maji vijijini  na usafi wa mazingira Ruwasa , mkimbiza mwenge wa uhuru kitaifa Ismaili Ally Ussi amesema sekta ya maji imekuwa ikitekeleza miradi katika kuzingatia ubora wa huduma ya maji safi na salama kwa mwananchi ambapo amewataka wananchi kuendelea kutunza miundombinu ya maji katika maeneo yao.

sauti ya mkimbiza mwenge wa uhuru kitaifa Ismaili Ally Ussi

Kwa upande wake Meneja wa Ruwasaa mkoa wa Manyara mhandisi James Kionaumela amesema mradi huo  utahudumia vijiji 21 pamoja na wananchi zaidi ya laki moja kunufaika na mradi huo wa maji ambapo amesema hadi sasa wamechimba visima 3 na upatikanaji wa maji utakuwa wa uhakika.

sauti ya Meneja wa Ruwasaa mkoa wa Manyara mhandisi James Kionaumela