FM Manyara

Wananchi zaidi ya 3,000 wanufaika na huduma ya maji Nadonjukin -simanjiro

13 July 2025, 11:04 pm

picha ya mradi wa maji

Zaidi ya wanachi 3,000 Katika Kijiji cha Nadonjukin wilaya ya simanjiro Mkoani Manyara wameondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta Maji baada ya Mwenge wa Uhuru kuzindua  mradi wa Maji  kutoka RUWASA  uliogharimu zaidi ya Shilingi Million miasita.

Na Emmy Peter

Akizungumza baada ya uzinduzi wa Mradi huo kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Ismaili Ally Ussi Ameipongeza Ruwasa kwa kuwa na Miradi ya kisasa inayo leta tija Kwa wananchi

Sauti ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa

Kwa upande wake Meneja wa wakala wa Maji na usafi wa mazingira vijijini(RUWASA) mkoa wa Manyara Injinia James Kiunaumela ameeleza mafanikio  ya Miradi hiyo  kwa wananchi, na kusema Ruwasa mkoa wa Manyara wamefika asilimia 78.9 kwa kuwafikishia huduma ya Maji safi na salama wananchi wa mkoa wa Manyara.

sauti ya Meneja wa Mamlaka ya Maji na usafi wa mazingira vijijini(RUWASA) mkoa wa Manyara Injinia James Kiunaumela

Aidha  wananchi Wa Kijiji cha Nadonjukin wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan   Kwa kuwaletea Mradi huo wa Maji kutoka Ruwasa kwani imesaidia kutatua changamoto iliyokuwa ikiwakabili kwa Muda Mrefu.