FM Manyara

Wananchi Magugu wafurahishwa utekelezaj ilani ya CCM

19 June 2025, 10:49 pm

Picha ya baadhi ya viongozi wa CCM na Diwani wa kata ya Magugu

Wananchi wa kata ya Magugu wilayani Babati mkoani Manyara, wameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuleta maendeleo katika kata hiyo kwa kuhakikisha inatatua changamoto ya maji, afya, bara bara, elimu na kilimo huku wakimpongeza diwani wa kata hiyo kwa kuhakikisha maendeleo yanapatikana.

Na Mzidalfa Zaid

Wananchi hao  wametoa pongezi hizo leo  baada ya kusomewa utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi kwa kipindi Cha miaka mitano kuanzia 2020/2025 .

Sauti ya baadhi ya wananchi wa kata ya Magugu

Awali afisa elimu kata Magugu Ally Msuya ambae amemuwakilisha afisa mtendaji wa kata hiyo, ameelezea utekelezaji wa chama cha mapinduzi kwa miaka mitano, ambapo amesema katika kipindi hicho serikali imefanikia kutatua changamoto ya maji, bara bara na sekta mbalimbali.

Sauti ya afisa elimu kata Magugu Ally Msuya

Kwa upande wake diwani wa kata ya Magugu Filbert Modamba  ameelezea namna  alivyojitoa katika kipindi chote cha uongozi na kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo.

Sauti yadiwani wa kata ya Magugu Filbert Modamba