Wakulima Manyara watakiwa kuacha kutegemea kilimo cha mvua
Wakulima Manyara watakiwa kuacha kutegemea kilimo cha mvua
7 May 2025, 12:56 pm
Meneja kutoka shirika la Kickstart Ernest Jerome aelezea jinsi kilimo cha umwagiliaji kilinavyoweza kumwinua mkulima mdogo na mkubwaa kwa kutumià vifaa ambavyo vitamwezesha mkulima kumwagilia kwa urahisi.
Na Angel Munuo
Wakulima mkoani Manyara wametakiwa kuacha kutegemea kilimo cha mvua pekee na badala yake kulima kilimo cha umwagiliaji ili kupata mazao ya uhakika na kujiongezea kipato.
Wito huo umetolewa na meneja kutoka shirika la kickstart Ernest Jerome alipokuwa akitoa elimu kwa wakulimà wa mkoa wa Manyara jinsi kilimo cha umwagiliaji kilinavyoweza kumwinua mkulima mdogo na mkubwaa kwa kutumià vifaa ambavyo vitamwezesha mkulima kumwagilia kwa urahisi.
Sauti ya meneja kutoka shirika la kickstart Ernest Jerome
kwa upande wake mwakilishi kutoka ofisi ya mkoa wa manyara Magreth wiza aliyekuwa mgeni rasmi,amesema kuna haja ya wakulimà kuvuna maji kipindi cha mvua ili kulima kilimo cha umwagiliaji hususani msimu wa kiangazi na kuacha kutegemea mvuaa ambayo haitoi matokeao mazuri katika kilimo kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
sauti ya mwakilishi kutoka ofisi ya mkoa wa manyara Magreth wiza
Aidha,wakulimà hao wamelipongeza shirika hilo kwa kuwapa elimu kuhusu kilimo cha umwagiliaji ambacho kitawasaidia kupata mazao ya uhakika katika misimu yotee na wataweza kujiongezea kipato kutokana na kilimo cha umwagiliaji.