FM Manyara

Zaidi ya wananchi 350 Manyara wapatiwa huduma ya macho

10 October 2024, 5:11 pm

Mganga mfawidhi wa hospital ya halmashauri ya mji wa Babati(Mrara) Dr Gillian Francis  Lupembe amesema Idadi ya wagonjwa waliokwenda kupata huduma ya matibabu ya macho  imekuwa kubwa kutokana na  watu wengi wanachangamoto  ya uoni.

Na Marino Kawishe

Zaidi ya wananchi Mia tatu hamsini wamepatiwa huduma ya uchunguzi wa macho kwenye hospital ya halmashauri ya mji wa Babati Mrara iliyopo mkoani Manyara kwenye clinic ya madaktari bingwa wa macho inayoendelea kwa siku mbili. 

Akizungumza na Fm Manyara Mganga mfawidhi wa hospital ya halmashauri ya mji mrara Dr Gillian Francis  Lupembe amesema Idadi hiyo imekuwa kubwa kwasababu watu wengi wanachangamoto ya uoni na wataendelea kushirikiana na madaktari bingwa kila wakati kutoa huduma kwa wananchi.

sauti ya Mganga mfawidhi wa hospital ya halmashauri ya mji mrara Dr Gillian Francis  Lupembe

Kwa upande wake meneja program kutoka KCCO ambao ni waratibu wa kambi hiyo ya madaktari bingwa kutoka hospital ya KCMC mkoani Manyara na hospital ya rufaa mkoani Manyara  Patricia Maaley amesema idadi hiyo inajumuisha watoto wa shule za msingi na sekondari ambao ni mia na hamsini na watu wazima zaidi ya mia mbili.

sauti ya meneja program kutoka KCCO

Nao baadhi ya wagonjwa waliojitokeza kupatiwa huduma za uchunguzi wa macho akiwemo mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Maisaka  Nikolaus  Marko  amesema wataanza kufanyia kazi utoaji wa  lishe bora kwa watoto  shuleni ili kuwakinga na magonjwa ya macho ambayo yanaweza kuepukika.

Sauti ya wagonjwa