FM Manyara

Mita za maji kuhakikiwa Manyara

August 21, 2024, 5:49 pm

Picha ya meneja wakala wa vipimo mkoa Manyara

Wakala wa vipimo mkoa wa Manyara wanatarajia kuanza msako wa kukagua mita za maji ili kubaini kama zinafanya kazi vizuri.

Na Mzidalfa Zaid

Wananchi mkoani Manyara  wametakiwa  kutoa taarifa  kwenye ofisi ya wakala wa vipimo ili zihakikiwe kama ziko sahihi wanapobaini  bili ya maji haiedani na matumizi ya maji wanayoyatumia.

Meneja  wa wakala wa vipimo mkoa wa Manyara Dennis  Misango amesema kwa sasa wanaendelea  na msako wa kukagua  na kuhakiki  mita hizo majumbani ili  kubaini  mita ambazo zinatoa majibu ambayo sio sahihi.

sauti ya meneja wakala wa vipimo Manyara

Amewataka wananchi kufahamu namna ya kusoma unit za maji ili kujua kama matumizi yao yanaenda na bili inayotolewa na mamlaka husika huku akiitaka mamlaka ya maji kuhakikisha wanasoma vizuri uniti zinazoonyesha kwenye mita hizo.