FM Manyara

      Wafanyabiashara Manyara watakiwa kutumia  EFD mashine

August 6, 2024, 6:51 pm

Picha ya Meneja  wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA  mkoa wa Manyara Joshua Mille (kulia) akiwa pamona na kaimu afisa elimu ya mlipa kodi TRA mkoa wa Manyara Ephraim Medad katika studio ya fm manyara radio

Imeelezwa kuwa lengo la kuanzishwa kwa mfumo  wa mashine za kieletroniki (EDF) mashine ni pamoja na  kumrahisishia mfanyabiashara utunzaji wa kumbukumbu za biashara kwasiku

 Na marino kawishe

Wafanyabiashara mkoani Manyara wametakiwa kuendelea  kutumia mashine za Kieletroniki(EFD)kwenye biashara zao ili kuondoa usumbufu wakati wa ukadiriaji wa kodi na kupunguza malalamiko yanayoweza kutokea wakati wa ukadiriaji wakodi ya mapato.

Meneja  wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA  mkoa wa Manyara Joshua Mille ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Trafick light kinachorushwa na kituo cha Fm Manyara radio,amesema  lengo la kuanzishwa kwa mfumo huo wa mashine za kieletroniki (EDF) mashine ni pamoja na  kumrahisishia mfanyabiashara utunzaji wa kumbukumbu za biashara kwasiku.

Sauti ya Meneja  wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA  mkoa wa Manyara

kwa upande wake kaimu afisa elimu ya mlipa kodi TRA mkoa wa Manyara Ephraim Medad amesema msambazaji anawajibu wa kuuza, kuwafungia na kuwafundisha matumizi sahihi ya mashine ambapo wafanyabiashara wanatakiwa kuwa na mashine hizo.

Sauti ya kaimu afisa elimu ya mlipa kodi TRA mkoa wa Manyara

Aidha,utaratibu wa kutumia mashine za kielectroniki (EFD) ulianzishwa rasmi mwaka 2010 kwa wafanyabiashara waliosajiliwa katika kodi ya ongezeko la thamani vat kwa utekelezaji wa sheria ndogo ya efd ya mwaka 2010.