FM Manyara

Manyara yajipanga kukuza uwezo wa wafanyabiashara

July 24, 2024, 5:37 pm

picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga amesema baada ya maonesho ya wafanyabiasha sabasaba  yaliyofanyika jijini Dar es salaam nakuwakutanisha  wafanyabiashara kinamama na taasisi inayojishughulisha na wakina mama wanaosafirisha bidhaa nje ya nchi wanatarajia kufanya mkutano na kinamama wazalishaji na wasafirishaji ili kujadili fursa mbali mbali na kusafirisha bidhaa nje.

Na George Agustino

Mkuu  wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga  amesema mkoa umejipanga kukuza uwezo wa wafanyabiashara wa ndani ya mkoa wa Manyara kwa kuwatoa na kuwashirikisha katika maonesho mbalimbali ya kibiashara ya nje na ndani ya mkoa watakayoanza  kuyaandaa.

  Sendiga ameyasema hayo leo julay 24 2024 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, amesema katika  maonesho ya wafanyabiashara sabasaba yaliyofanyika jijini Dar es salaam kitaifa kwa mwaka 2024 mkoa wa Manyara umeshiriki na wafanya biashara wa ndani ya mkoa walioshiriki ambapo wamepata manufaa makubwa kwa kutangaza na kuuza bidhaa zao pamoja na kupata masoko ya nje ya nchi .

sauti ya mkuu wa mkoa wa Manyara

Aidha Sendiga amesema kupitia maonesho hayo ya sabasaba wamewaunganisha wafanyabiashara kinamama na taasisi inayojishughulisha na wakina mama wanaosafirisha bidhaa nje ya nchi ambapo wanatarajia kufanya mkutano na kinamama wazalishaji na wasafirishaji ili kujadili fursa hizo za kusafirisha bidhaa nje.

sauti ya mkuu wa mkuu mkoa Manyara