FM Manyara

Wakulima mkoani Manyara  watakiwa kuuza  Mazao kwa kutumia Mizani

June 13, 2024, 4:47 pm

Wakala wa vipimo mkoa wa Manyara unajukumu la kumlinda mlaji kwa kupima mizani zote za wafanyabiashara ili mkulima auze mazao yake na kupata fedha kulingana na thamani ya mazao yake aliyolima

Na George Augustino

Wakulima mkoani Manyara wametakiwa kuuza mazao mbali mbali  kwa Wafanyabiashara kwakutumia mizani zilizohakikiwa na wakala wa vipimo mkoani hapa  na  kuachana na vipimo batili ili kuepuka kuibiwa na wafanyabiashara hao.

 Meneja wa vipimo mkoa wa Manyara Denis Misango ameyasema hayo wakati akizungumza na Fm Manyara amesema jukumu lao kubwa ni kumlinda mlaji kwa kupima mizani zote za wafanyabiashara ili mkulima auze mazao yake na kupata fedha kulingana na thamani  ya mazao aliyouza .

Sauti ya Meneja Wakala wa Vipimo Manyara

Aidha Misango amesema mazao yote yanayonunuliwa yanatakiwa kufungashwa  kwa uzito unaokubalika kwa mujibu wa sheria ya vipimo  ambapo mazao yote ya shambani yanatakiwa kufungashwa kwa uzito usiozidi kilo 100 na gunia likizidi kilo105 ni kosa kisheria na mfanyabiashara huyo anatakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria

Sauti ya Meneja Wakala wa Vipimo Manyara